Tangaza nasi DvJGaby.Blogspot,com

Tangaza nasi DvJGaby.Blogspot,com

Wednesday, 11 November 2015

MSANII WA BONGO FLAVE STEVE RNB ANAKUJA NA NYIMBO MPYA


Ni staa wa bongofleva ambae hits zilizompa headlines ni pamoja na ‘Tabasamu‘ aliyoshirikishwa na Mr. Blue, msanii huyo  tangu afunge ndoa October 11 2014 amekuwa kimya katika tasnia ya Bongo Fleva sasa hapa ameyajibu yote.

Akiongea na ripota wa millardayo.com msanii huyo alisema..’Ni kitu cha kawaida kwani kuoa ni kama kutoka stage moja na kwenda nyingine ila sio kama nimekuwa kimya sana bali kuna baadhi ya mashabiki wangu wanakuwa wananiona kwenye muziki wa bendi  na mpaka sasa nipo na bendi iitwayo Ina Afrika Band kuna project nilikuwa nazunguka nao iitwayo Mama Africa inafanyika nchi za nje kama Ulaya’- Steve RNB
‘Lakini sio kama ni kweli kwamba tangu niingie kwenye ndoa basi ndio imenifanya ni stop lakini this time mashabiki nimetenga muda wao kwaajili ya kufanya muziki wa Bongo Fleva ukiachana na muziki ninaoufanya kwa sasa wa Bendi kwa hiyo soon mambo yote yatakuwa mazuri’ – Steve Rnb

No comments:

Post a Comment